186. Kama ulivyoagiza

1 Kama ulivyoagiza
kabla kuuawa,
hivi nitafanya Bwana,
nitakukumbuka.

2 Wewe kwa ajili yangu
ulitoa mwili,
katika mkate wako huu,
nitaukumbuka.

3 Vivyo damu ya thamani
wewe ulitoa.
Katika kikombe hiki
nitaikubuka.

4 Nitazamapo Golgota,
kuona msalaba,
na kipaji cha kafara
nitakikumbuka.

5 Siwezi kusahau jinsi
ulivyoumia,
kweli nikiwapo mzima
nitakukumbuka.

6 Kwa hiyo nakungojea
ee Bwana, kwa kuwa
ujapo mara ya pili,
utanikumbuka.

Text Information
First Line: Kama ulivyoagiza
Title: Kama ulivyoagiza
English Title: According to Thy gracious word
Author: J. Montgomery (1825)
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Chakula cha Bwana
Notes: Sauti: Martyrdom by H. Wilson, Lutheran Book of wotship #98, Service Book and Hymnal #486, Hymnal Companion #323
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us