Text: | Wakristo, iwekeni |
Author: | V. Thilo, 1607-1662 |
1 Wakristo, iwekeni
mioyo tayari.
Yesu awaingie,
ni Mwokozi wenu.
Mungu amemtuma
kwa neema na rehema
atuletee sisi
uzima na nuru.
2 Mwokozi anakuja,
mlimieni njia!
Mioyo iwe safi
acheni matendo
yanayomchukiza.
Lijazwe kila bonde,
milima ipunguzwe
mioyoni mwenu.
3 Ukiwa mnyenyekevu,
Wapendwa na Mungu.
Ukiwa na kiburi,
utaangamizwa.
Ukimtumikia
Mungu kwa Mwendo mwema
umpendezao yeye,
Yesu akupenda.
4 Uniwke tayari,
niliye maskini,
Ee Yesu, siku hizi
kwa rehema yako,
Ingia moyoni,
ukinijia sasa.
Nami nitakusifu
kwa kinywa na moyo.
Text Information | |
---|---|
First Line: | Wakristo, iwekeni |
Title: | Wakristo, iwekeni |
German Title: | Mit Ernst, o Menschenkinder |
Author: | V. Thilo, 1607-1662 |
Language: | Swahili |
Publication Date: | 1988 |
Notes: | Sauti yake: Namba 206; Posaunen Buch, Erster Band #5 and #94 |