185. Mfalme wa upendo ndiye

1 Mfalme wa upendo ndiye
anichungaye mimi,
yeye ni wangu milele,
ananipenda daima.

2 Kando ya maji uzima
hunipeleka mimi
katika malisho mema,
anilisha siku zote.

3 Mara nyingi napotea
kwa ukaidi wangu,
naye ananitafuta,
na kunirudisha kwake.

4 Kivuli cha kufa kwangu
sitaogopa Bwana,
ukiwa kwangu daima
masaka wayaondoa.

5 Wanitandikia meza,
naula mkate wako,
nanywa katika kikombe
nikumbuke kufa kwako.

6 Siku zangu zote hapa
wema wako u vivyo.
Nikubali Mchunga mwema,
nikuimbie milele.

Text Information
First Line: Mfalme wa upendo ndiye
Title: Mfalme wa upendo ndiye
English Title: The king of love
Author: H. W. Baker, 1821-1877
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Chakula cha Bwana
Notes: Sauti: Dominus regit me by J. B. Dykes, 1832-1867, Service Book and Hymnal #530
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us