205. Kuna nchi nzuri

1 Kuna nchi nzuri mbali sana.
Wako watu wema, wasimama,
waimba vizuri sifa zake Mwokozi,
nasi duniani twamtukuza.

2 Njooni kwa nchi hii njooni sasa!
Mbona mwasimama mashakani?
Tuache makosa, yanamchukiza Bwana,
Kwake tutaketi kwa salama.

3 Machozi hapana, wala hamu,
mbele yake Baba mapenzi tu.
Utaona raha utapewa kilemba
kuvikwa na wale wa mbinguni!

Text Information
First Line: Kuna nchi nzuri
Title: Kuna nchi nzuri
English Title: There is a happy land
Author: A. Young
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kufa na kuzikwa
Notes: Sauti: Happy land, Asili: Amerika, Hymnal Companion #512
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us