1 Nemo lako, Bwana,
Ni imara sana;
Hilo latuongoza,
Hilo latufunza.
2 Adui wabaya
Wakikaribia,
Neno lake Bwana
Ni ulinzi sana.
3 Siku za dhoruba
Soma ukiomba;
Neno lake Bwana
Msaada sana.
4 Ukiliamini,
Huenda na amani;
Una na furaha:
Neno ni silaha.
5 Ni furaha kweli,
Na wingi wa mali,
Neno lake Bwana
Kwa wasiokana.
6 Neno la rehema,
Tungali wazima;
Faraja i papo,
Tufarakanapo.
7 Tulijue sana
Neno lako, Bwana,
Hapa tukupende,
Kisha kwako twende.
Text Information | |
---|---|
First Line: | Nemo lako, Bwana |
Title: | Neno lako, Bwana ni imara |
English Title: | Lord, thy word abideth |
Language: | Swahili |
Publication Date: | 1988 |
Topic: | Kumtambikia Mungu: Sikukuu za Wakristo |
Notes: | Sauti: Lord, thy word abideth, Hymnal Companion #267, G.N. #584, English Hymnal #436 |