247. Neno lako, Bwana ni imara

1 Nemo lako, Bwana,
Ni imara sana;
Hilo latuongoza,
Hilo latufunza.

2 Adui wabaya
Wakikaribia,
Neno lake Bwana
Ni ulinzi sana.

3 Siku za dhoruba
Soma ukiomba;
Neno lake Bwana
Msaada sana.

4 Ukiliamini,
Huenda na amani;
Una na furaha:
Neno ni silaha.

5 Ni furaha kweli,
Na wingi wa mali,
Neno lake Bwana
Kwa wasiokana.

6 Neno la rehema,
Tungali wazima;
Faraja i papo,
Tufarakanapo.

7 Tulijue sana
Neno lako, Bwana,
Hapa tukupende,
Kisha kwako twende.

Text Information
First Line: Nemo lako, Bwana
Title: Neno lako, Bwana ni imara
English Title: Lord, thy word abideth
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kumtambikia Mungu: Sikukuu za Wakristo
Notes: Sauti: Lord, thy word abideth, Hymnal Companion #267, G.N. #584, English Hymnal #436
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us