Text: | Nataka kusimama |
Author: | E. C. Clephane, 1830-1869 |
1 Nataka kusimama
chini ya msalaba,
kama kivuli cha mwamba
wakati wa mchana,
kama ni maji nyikani,
kambi safarini,
na hapa nitapumzika,
kwani jua kali.
2 Mahali pema sana
chini ya msalaba,
kwani hapo waoneka
upendo wa Yesu.
Yakobo alivyoona
ndotoni zamani,
mti Yesu aliowambwa,
ni ngazi kwa Mungu.
3 Juu ya msalaba huo
Yesu alikufa.
Alikufa tuokoke,
tuliopotea.
Ninastaajabu kabisa
ni mambo mawili:
kwake Yesu ni upendo,
kwangu mimi kosa!
4 Wataka kuonana
na Yesu mbinguni,
yakupasa kukaa kwanza
chini ya mti huo.
Ni kweli siku chache tu
mateso na shaka.
Halafu pasipo mwisho
furaha kwa Bwana!
Text Information | |
---|---|
First Line: | Nataka kusimama |
Title: | Nataka kusimama |
English Title: | Beneath the cross of Jesus |
Author: | E. C. Clephane, 1830-1869 |
Language: | Swahili |
Publication Date: | 1988 |
Topic: | Kuteswa na kufa kwa Yesu |
Notes: | Sauti: Beneath the cross of Jesus by C. D. Sankey, 1840-1908 and F. C. Maker 1844-1927, Reichs Lieder #263, Lutheran Book of Worship #107 |