1 Nikulakije vema
Bwana wangu Yesu?
Wote wanakungoja
wapewe uzima.
Nuru yako ing’aze
hata moyo wangu,
nijue mambo mema
yakupendezayo.
2 Wamekutandikia
maua na nguo.
Nami nakuimbia
nyimbo za furaha.
Moyo ukupendeze
kwa sifa na nyimbo,
ukakutumikie
siku zangu zote.
3 Umetoka mbinguni
ukawa maskini.
Ukaacha furaha
utupe uzima.
Na tuliponyang’anywa
ufalme na raha,
ukaja mponya wetu
kuturudishia.
4 Nalifungwa na mwovu,
ukanifungua.
Nikawa nimetwezwa,
ukanifanya,
Ukanifanya mkubwa,
ukanipa mali,
zisizomalizika
kwa kutu na wezi.
5 Umenijia mimi
sababu ya nini?
Sababu ya kupenda,
uwaponye wote
waonao huzuni
kwa makosa yao.
Wakijuta kwa kweli
utawapokea.
6 Ushike neno hili,
Umati wa Yesu,
ukiwa na huzuni
na shida popote.
Usiogope kitu:
wokovu tayari.
Anayetufariji
yu karibu sasa.
Source: Mwimbieni Bwana: msifuni Mungu, mfalme wa mbingu na nchi! #5