246. Namwandama Bwana

1 Namwandama Bwana
kwa alilonena,
Njia yangu huning'azia;
Nikimridhisha atanidumisha
Taamini nitii pia.

Refrain:
Amini utii
njia pekee ni hii
Ya furaha kwa Yesu:
amini ukatii.

2 Giza sina kwangu
wala hata wingu.
Yeye mara huviondoa
Woga, wasiwasi,
sononeko, basi;
Huamini natii pia. [Refrain]

3 Masumbuko yote,
sikitiko lote;
Kwa mapenzi hunilipia;
Baa, dhara, dhiki,
vivyo hubariki.
Niamini nitii pia. [Refrain]

4 Mimi sitajua
raha sawasawa
Ila yote Yesu anipa;
Napata fadhili
na radhi kamili,
Niamini nitii pia. [Refrain]

5 Nitamfurahia
na kumtumaini,
Safarini hata nyumbani;
Agizo natenda;
nikitumwa huenda,
Huamini natii pia. [Refrain]

Text Information
First Line: Namwandama Bwana
Title: Namwandama Bwana
English Title: When we walk with the Lord
Refrain First Line: Amini utii
Language: Swahili
Publication Date: 1988
Topic: Kumtambikia Mungu: Sikukuu za Wakristo
Notes: Sauti: When we walk with the Lord, L.S. #211, Sacred Songs and Solos #542, R.S. #495
Tune Information
(No tune information)



Suggestions or corrections? Contact us