Author: K. H. v. Bogatzky, 1690-1774 Appears in 1 hymnal Lyrics: 1 Uamke kwetu tena Roho
ya mashahidi wale wa kwanza,
waliokesha siku zote,
waliomshinda yule adui,
wakihubiri neno la Yesu
kwa watu wa ulimwengu wote.
2 Uwashe moto wa upendo,
uendelee pote kuwaka.
Peleka watu mavunoni,
wanaofanya kazi kwa bidii.
Bwana mwenye mavuno, tazama:
Watenda kazi yako ni haba.
3 Mwanao ametuaqiza
kuomba hivi kwa jina lake,
na sisi wanafunzi wake,
twashika neno lake kwa bidii.
Twaomba hivi kwa moyo wote.
Ee Bwana usikie, ufanye!
4 Utame watu wengi sana,
walitangazi neno kwa nguvu.
Usaidie tuokoe,
ufalme wa Shetani uishe.
Usimamishe, Bwana wa mbingu,
ufalme wako ulimwenguni!
5 Uteme mwema na uende
mahali popote huku nchini,
wamizimu na waingie
kundini mwako mwa wateule.
Amsha nao Waisraeli
na Waislamu waje, wakutii. Topics: Epifania, Mission
Uamke kwetu tena Roho