15524. Tangu Siku Hijo Aliponijia

1 Tangu siku hiyo aliponijia,
Akae moyoni mwangu.
Sina giza tena, ila mwanga pia,
Kwa Yesu, Mwokozi wangu.

Refrain:
Amani moyoni mwangu,
Kwa Yesu, Mwokozi wangu.
Sina shaka kamwe
Kwa sababu yeye
Yu nami moyoni mwangu.

2 Sina haja tena ya kutanga-tanga,
Ndiye Kiongozi changu.
Dhambi zangu zote zimeondolewa,
Na Yesu Mwanawe Mungu. [Refrain]

3 Matumaini yangu ni ya hakika,
Katika Mwokozi wangu.
Hofu zangu na hamu zimeondoka,
Kwa kuwa ninaye Yesu. [Refrain]

4 Siogopi tena nikiitwa kufa,
Yu nami daima Yesu.
Mlango wa mbingu ni Yesu Mwokozi,
’Tapita humo kwa damu. [Refrain]

5 Nitaketi na Yesu huko milele,
Nimsifu Mwokozi wangu.
Nina raha moyoni majira yote,
Kwa Yesu Mwanawe Mungu. [Refrain]

Text Information
First Line: Tangu siku hiyo aliponijia
Title: Tangu Siku Hijo Aliponijia
English Title: What a wonderful change in my life has been wrought
Author: Rufus Henry McDaniel
Translator: Unknown
Refrain First Line: Amani moyoni mwangu
Language: Swahili
Copyright: Public Domain
Tune Information
Name: [Tangu siku hiyo aliponijia]
Composer: Charles Hutchinson Gabriel
Key: A Major
Copyright: Public Domain



Media
MIDI file: PDF
More media are available on the tune authority page.

Suggestions or corrections? Contact us